KATIBU MKUU CCM
KINANA.
JOSEPH WALIOBA.
MFUMO wa
serikali tatu uliopendekezwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba unaonyesha
dhahiri kukichanganya Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Mfumo huo
ulipendekezwa katika rasimu ya Katiba mpya iliyozinduliwa Jumatatu ya wiki
iliyopita na Tume ya Mabadiliko ya Katiba imayoongozwa na jaji mstaafu, Joseph
Warioba.
Tume hiyo
ilipendekeza kuun
dwa kwa
serikali za Shirikisho, Tanzania Bara na ya Zanzibar huku ikiainisha mambo saba
ambayo yatashughulikiwa na serikali hiyo..
Baada ya tume hiyo kutoa mapendekezo yake katika rasimu hiyo, makundi
mbalimbali ya jamii yanahoji pendekezo la mfumo wa Muungano wa serikali
hususani uundwaji wake na uendeshaji.
Miongoni mwa mambo yanayohojiwa ni muundo wenyewe, kiongozi mkuu wa
serikali ya Tanganyika ataitwa Rais au waziri Mkuu, je, atakuwapo Makamu wa
Rais.
Baadhi ya
watu wanasema serikali tatu zitahitaji kuendeshwa kwa gharama kubwa na kuhoji
serikali ya Shirikisho itaendeshwa kwa mapato gani wakati mapato yatakuwa
yanakusanywa na serikali za Zanzibar na Tanzania Bara.
Lipo pia
suala la utawala kwamba Rais wa Shirikisho anaposafiri au kupata udhuru ni nani
atakaimu madaraka yake. Wengine wanahoji nani atakuwa na madaraka makubwa kati
ya Rais wa Tanzania bara na Zanzaibar.
Wako
wanaohoji kwamba ni utaratibu upi utawekwa kwa ajili ya watu wanaotaka kugombea
urais wa Shirikisho, Zanzibar na Tanzania Bara.
Baadhi ya
watu wanaoupigia hesabu urais mwaka 2015 kauli wanazozitoa zinaonyesha wazi
kuwa wameingiwa na hofu kutokana na kushindwa kuelewa wagombee wapi.
Haya yote na
mambo mengine yenye utata ndiyo yanayosababisha makundi mbalimbali ya jamii
kuhoji mambo mengi kuhusiana na suala la mfumo wa serikali tatu.
Hata hivyo,
CCM ambacho sera yake ya mfumo wa Muungano ni serikali mbili, kimejikuta katika
wakati mgumu wa kuamua.
Kwa kuwa ni
suala la sera, chama hicho tawala kitapaswa kwenda kwa wanachama wake kupata
maoni yake kabla ya kuridhia mfumo wa Muungano wa serikali tatu.
Ni dhahiri
kwamba ikiwa wanachama wa CCM watakataa pendekezo la mfumo wa serikali chama
hicho ambacho ndicho kinachounda serikali kitatumia ushawishi wake katika vyombo
vya maamuzi likiwamo Bunge kulikataa pendekezo hilo.
Chama
hicho kina idadi kubwa ya wabunge katika Bunge Maalum la Katiba, lakini pia
Mwenyekiti wake, Rais Jakaya Kikwete ndiye kiongozi mkuu wa nchi ambaye
atakabidhiwa rasimu hiyo kabla ya kupigiwa kura ya maoni na wananchi.
Katika
hatua inayoonyesha kuwa chama tawala kinajipanga kabla ya kutoa msimamo
wake, Kamati Kuu (CC) ya CCM leo itakutanakujadili suala hilo.
Wiki
iliyopita, chama hicho kilitangaza kwamba CC itakutana leo kujadili mapendekezo
ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba huku kikisema kuwa hakiyaungi mkono kwa
asilimia mia moja mapendekezo yaliyomo kwenye rasimu.
Kauli hiyo ya
chama tawala ilitolewa na Katibu Mkuu wake, Abdulrahman Kinana, baada ya
kuulizwa na waandishi wa habari kuhusu msimamo wa chama chake juu ya rasimu
mpya.
Kinana
alisema uamuzi wa kutangaza msimamo wa chama utatokana na kikao cha CC),
kitakachokutana leo chini ya mwenyekiti wake, Rais Kikwete.
“Kwa sasa
hatuungi mkono rasimu hii kwa asilimia 100 wala kuipinga mpaka hapo tutakapokaa
CC wiki ijayo (leo) na kuamua msimamo wetu ni upi katika hili,” alisema
Kinana.
Alisema kila
jambo ndani ya chama hicho huamuliwa kwa pamoja kupitia vikao na kwamba huo
ndio utaratibu wao.
Wachambuzi wa
mambo ya siasa wanaichukulia kauli ya Kinana ya kutounga mkono mapendekezo ya
rasimu kwa asilimia mia moja kuwa alikuwa anamaanisha kwamba pendekezo kuhusu
mfumo wa serikali tatu hawakukubaliani nalo.
Baadhi ya
vigogo wa CCM wametoa maoni ambayo yanaonyesha wazi kuwa ndani ya chama hicho
kuna mgawanyiko kuhusiana na suala hilo.
Mjumbe wa
Halmashauri Kuu (NEC) ambaye pia ni Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Samuel Sitta, anasema kuwa mchakato wa rasimu ya katiba umelenga kuvuruga
Muungano na kuibebesha mzigo serikali.
Waziri Mkuu
mstaafu, Frederick Sumaye, anasema mfumo wa serikali tatu ni gharama kubwa
ikilinganishwa na hali halisi ya pato la nchi.
Warioba
ambaye ni Waziri Mkuu mstaafu, anasema kama mfumo wa serikali tatu utakubalika,
serikali ya Muungano haitakuwa na haja ya kukopa fedha na katika suala la
uwakilishi wan chi kimataifa, Rais wa Muungano ndiye atakuwa na jukumu hilo na
siyo Rais wa Tanzania Bara au wa Zanzibar.
Waziri Mkuu
mstaafu, John Malecela, anatahadharisha kuwa lazima suala la serikali tatu
liangaliwe kwa umakini lisije kuleta matatizo.
Kauli hizo
zinazokinzana, zinadhihirisha kuwa ajenda ya mfumo wa Muungano itazua mjadala
mkali katika kikao cha leo cha CC.
Mfumo wa
Muungano ni moja ya mambo ambayo serikali ya CCM imekuwa ikiyachukulia maamuzi
kwa uangalifu mkubwa kama sera ya chama hicho.
Maoni
yanayotolewa na vigogo wastaafu ynaweza kuleta ushawishi kwa vigogo wa CCM na
kuamua kuitupa hoja ya serikali tatu kwa kuhofia yaliyowapata baadhi ya
viongozi walioathiriwa na kushabikia mfumo wa serikali tatu.
Rais
mstaafu wa Zanzibar, Alhaji Aboud Jumbe, mwaka 1984 alivuliwa nafasi zake zote
za uongozi kutokana na kutaka mfumo wa serikali tatu.
Mapema miaka
ya 90 suala la Muungano liliitikisa serikali ya awamu ya pili ya Ali Hassan
Mwinyi, ilijikuta katika mtikisiko mkubwa, baada ya kuridhia kuundwa kwa
serikali ya Tanganyika ndani ya Muungano.
Uamuzi huo
ulitokana na shinikizo la kundi la wabunge 55 maarufu kwa jina la G55 ambalo
lilikuwa linapinga uamuzi wa Zanzibar kuamua kujiunga na Jumuiya ya Kimataifa ya
Kiislamu (OIC) kinyume cha Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Baada ya
Bunge kupitisha hoja hiyo na serikali kuridhia, Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu
Julius Nyerere, aliingilia kati kwa na kuwaambia wabunge wakiokuwa
wakishinikiza kuundwa kwa serikali ya Tanganyika kusitisha hoja hiyo au
wajiondoe ndani ya CCM.
Aliyekuwa
waziri Mkuu, John Malecela na Katibu Mkuu wa CCM, Hayati Horace Kolimba,
walivuliwa nyadhifa zao kwa madai ya kumshauri vibaya Mzee Mwinyi.
Wakati wa
uongozi wa awamu ya tatu wa Rais Benjamin Mkapa suala la mfumo wa Muungano
liliibuka upya, lakini alitumia nguvu kuzima mawazo ya kutaka serikali
mbili.
Hata
alipounda Tume ya kukusanya maoni chini ya uenyekiti wa Jaji Robert Kisanga
kupitia utaratibu wa waraka maalum wa White Paper, Mkapa alikataa mapendekezo
ya tume hiyo ya kupendekeza mfumo wa serikali tatu, akiwatolea lugha kali
wajumbe wa tume kuwa hawakupewa adidu ya kutoa mapendekezo bali kukusanya maoni
kuhusu Muungano.
MBOWE: KIFO
CHA CCM CHAJA
Wakati huo
huo; Mwenyekiti wa Chama Cha Demokreasia na Maendeleo (Chadema) Taifa, Freeman
Mbowe, amesema CCM kimefikia ukomo wake kufuatia katiba mpya ambayo rasimu yake
imetolewa na tume ya katiba hivi karibuni.
Akizungumza
jana na wakazi wa Kata ya Iyela jijini Mbeya katika kampeni za uchaguzi mdogo
wa kata ya hiyo ambao unatarajiwa kufanyika Juni 16 mwaka huu, alisema kufuatia
muundo wa katiba inayokuja, CCM inaelekea kufa kutokana na katiba hiyo kuruhusu
mgombea binafsi na serikali tatu.
Alisema kuwa
viongozi wa chama hicho wamekuwa wakila fedha za walipa kodi wakiwa madarakani
na ndiyo maana wamekuwa wakiutafuta uongozi kwa kasi kubwa.
CHANZO:
NIPASHE.
No comments:
Post a Comment