ADV

ADV

ADVERTISEMENT CORNER

HUDUMA YA KUKATA TICKET ZA NDEGE ONLINE


SOMA HABARI

SOMA HABARI

Sunday, June 2, 2013

panis triticeus et vinum de vite

 
Papa Francis akibariki waumini kwa Ekaristi Takatifu
 
Wakristo wakibeba hema lililofunika Padre aliyebeba Monstrance yenye Ekaristi Takatifu.
panis triticeus et vinum de vite (ngano na mzabibu) ambavyo ndivyo elements vinavyotumika katika kugeuzwa kuwa Mwili na Damu ya Yesu
Huu ndio mwili wangu; hii ndiyo damu yangu. Jumapili hii tunaadhimisha Siku kuu ya Mwili na Damu ya Kristo. Siku kuu yeneyewe yatusaidia kutafakari juu ya umoja uliopo baina yetu na Kristo, kwani sisi tu viongo vya mwili wake. Kwenye Mkutano Mkuu wa Sinodi ya Maasikofu wa Afrika, Sinodi ilisema, "Kanisa bara letu Afrika tu Jamaa ya Mungu". Twajua kwamba pakiwa na umoja kwenye familia, pia kuna ushirikiano. Hivyo pia, viungo vya mwili vikiwa na ushirikiano, mwili mzima hupata nguvu, utulivu na furaha. Lengo la siku kuu hii hasa ni kuonyesha umoja wetu na furaha yetu katika Kristo, anayetupatia mwili wake na damu yake, kama chakula cha uzima. Kwenye Somo la kwanza twasikia jinsi Mungu alivyofanya agano lake na wana wa Israeli. Mungu aliwapa amri za wokovu, na Waisraeli walihahidi kuzitimiza kwa kudhihirisha agano hilo kwa damu ya wanyama. Somo la pili yatuonyesha jinsi Mungu alikamilisha agano lake na kuilitia muhuri kwa damu ya Mwanae ili kutakasa roho zetu. “Kwa damu ya Kristo, mambo makuu zaidi hufanyika!”. Injili ya siku kuu hii yatuonyesha Yesu akifanya mujiza wa kuzidisha mikate 5 na samaki 2, ili umati wa watu wale. Tunasikia kwamba wote walikula na wakashiba. Lengo hasa ya kula pamoja ni kutuonyesha jinsi Mungu uwashibisha waku wake wote bila kubagua. Hivyo pia ndiyo ishara kubwa la Sakramenti kuu ya Ekaristi.

Hivyo sherehe za Ekaristi katika Misa takatifu ni kiini cha umoja wetu na Kristo unaofikia kilele chake wakati wa Komunio Takatifu. Lakini ijapokuwa Ekaristi yatulisha ki-roho, huenda tukasahahu jinsi Ekaristi inao upande wa kuzingatia haki za ki-binadamu. Sherehe za Mwili na Damu ya Kristo ndio wakati unaofaa wa kutafakati na kutia maanani jinsi Ekaristi inahusiana na haki. Wakati wa Mwaka wa Jubileo ya Ekaristo Oktoba 2004 hadi Oktoba 2005, Baba Mtakatifu, Yohane Paulo II kwenye Barua yake Mane Nobiscum Domine (Bwana Kaa Nasi) alisema: “Si tungefanya Mwaka huu wa Ekaristi wakati ambao kila Jimbo na kila Parokia kujiazimia kwa njia ya pekee kujihusu na mojawapo ya aina za umasikini duniani? Baba Mtakatifu alionya kwamba “Kigezo kitakaothibitisha sherehe zetu za Ekaristia Takatifu kitakuwa upendo wetu kwa wenzetu na hasa kujishugulisha na wale wasiojiweza.” Mtakatifu Paulo amesema kwamba Jumuiya ya Kikristo “haifai” kusherekea Karamu ya Bwana baina ya ugawanyifu na kutowajali masikini (1 Kor. 11:17-22, 27-34). Katekisimu ya Kanisa Katoliki yatuambia: “Kupokea kwa ukweli Mwili na Damu ya Kristo aliyotutolea, yatulazimu kumgudua Kristo katika masikini wa mwisho, ndugu yake.” (Na. 1397). Sherehe ya Mwili na Damu ya Kristo hukumbukwa hasa kwa sababu ya maandamano ya kuvutia ya Ekaristi. Maandamano hayo pia ni wito kwetu ili kama Kristo nasi pia tuwe tayari kumwaga damu yetu kwa ajili ya wengine. Wakati wa ubaguzi wa rangi huko Namibia, Kanisa Katoliki ilitumia maandamano ya Siku kuu hii, kama ishara ya kuwepo kwa Kristo baina ya watu, wakati wanaotetea haki zao. Ekaristi basi ilikuwa ukumbusho wa kweli wa kujitoa kwa Kristo msalabani ili kuondoa nyororo za dhambi na ukatili. Kuna ujumbe gani tungepeleka nyumbani? 1) Ekaristi ni ukumbusho wa kweli kuhusu sadaka aliyotoa Kristo ili kutukomboa sisi zote kutoka chochote kinachowakatili binadamu, hasa sana kutokana na dhambi. 2) Hivyo, ndio sababu sherehe za Mwili na Damu ya Kristo katika nchi za kiukatili zatoa ushuhuda mkali na kuudhiwa na serikali dhalimu kama kule Namibia wakati wa ubaguzi wa rangi. 3) Sherehe za Mwili na Damu ya Kristo haziwezi kutenganishwa na udhalimu uliopo kwenye jumuiya yetu, kwa sababu uadhimisho wa Ekaristi ni utangazaji wa haki za wanaodhalimiwa. 4) Basi Siku kuu ya leo itathibitishwa uaminifu wetu ikiwa tutawakumbuka hasa wale wasio na chakula na cha kunywa, yaani wote ndugu na dada za Bwana wetu Yesu Kristo.


©2013 John S. Mbinda

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...