ADV

ADV

ADVERTISEMENT CORNER

HUDUMA YA KUKATA TICKET ZA NDEGE ONLINE


SOMA HABARI

SOMA HABARI

Monday, July 15, 2013

Mh. Mbowe afika Polisi Makao Makuu kwa mahojiano





Kwa wale ambao mnakumbuka kuwa siku ya ijumaa usiku wa manane Polisi kutoka Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni wakiongozwa na RCO wa Kinondoni walienda nyumbani kwa Mbowe majira ya saa saba usiku kwa lengo la kumkamata, Mbowe alikuwa safarini na alipitia Airport ya Dsm Hivyo kwenda kwake usiku ni jambo la kushangaza sana , leo amerejea kupitia Airport ya Dar na akaamua kwenda moja kwa moja Polisi ili kujua kulikoni.

Ameambatana na Mawakili wawili, Nyaronyo Kicheere na Peter Kibatala majira ya saa tisa na nusu aliingia Makao Makuu ya Polisi na huko wanaendelea na Majadiliano.

Jambo la kushangaza ni kuwa mahojiano yao yanahusu mambo yafuatayo;

1. Kuwa tamko la Kamati Kuu kuwa Polisi walihusika na mlipuko wa Bomu Arusha... Itakumbukwa alishahojiwa tena na akina Chagonja na mpaka leo hakuna taarifa zozote wazi.
2. Kuwa Polisi wanatumiwa na CCM ndio maana wanaisaidia CCM Katika chaguzi mbalimbali ......na hata bomu la Arusha ilikuwa sehemu ya mkakati huo.
3. Kwamba kauli kuwa JK na Bunge kutokuonyesha dalili zozote za kusikitishwa na hata kushindwa kuhudhuria mazishi ni dalili za serikali kuhusika katika tukio hilo.
source jamii forum

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...