ADV

ADV

ADVERTISEMENT CORNER

HUDUMA YA KUKATA TICKET ZA NDEGE ONLINE


SOMA HABARI

SOMA HABARI

Wednesday, August 28, 2013

KUTOKA JESHI LA POLISI TANZANIA:SOMA TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI KIDATO CHA NNE NA SITA 2013.


Jeshi la Polisi Tanzania limetoa majina na ratiba ya usahili kwa vijana waliomaliza kidato cha nne mwaka 2012 na waliomaliza kidato cha sita mwaka 2013 ambao wamechaguliwa kufanya usaili kabla ya  kujiunga na Jeshi la Polisi.

Mikoa, vituo na tarehe za usaili zimeoneshwa kwenye jedwali hapa chini:
NA
MIKOA
KITUO CHA USAILI
TAREHE ZA USAILI
MUDA WA  USAILI
1
KILIMANJARO  NA TANGA OFISI YA RPC TANGA 02-04 /09/2013 08:00 ASUBUHI -16:00 JIONI
2
MANYARA NA ARUSHA OFISI YA RPC ARUSHA 06-09 /09/2013 08:00 ASUBUHI -16:00 JIONI
3
RUVUMA  NA NJOMBE OFISI YA RPC NJOMBE 12-14 /09/2013 08:00 ASUBUHI -16:00 JIONI
4
IRINGA NA MBEYA OFISI YA RPC MBEYA 16-18 /09/2013 08:00 ASUBUHI -16:00 JIONI
5
RUKWA NA KATAVI OFISI YA RPC RUKWA 20-23 /09/2013 08:00 ASUBUHI -16:00 JIONI
6
MTWARA NA LINDI OFISI YA RPC MTWARA 26-28 /09/2013 08:00 ASUBUHI -16:00 JIONI
7
KIGOMA OFISI YA RPC KIGOMA 02-04 /09/2013 08:00 ASUBUHI -16:00 JIONI
8
MWANZA NA MARA OFISI YA RPC MARA 06-09 /09/2013 08:00 ASUBUHI -16:00 JIONI
9
GEITA NA KAGERA OFISI YA RPC  GEITA 12-14 /09/2013 08:00 ASUBUHI -16:00 JIONI
10
SHINYANGA NA SIMIYU OFISI YA RPC SHINYANGA 17-19 /09/2013 08:00 ASUBUHI -16:00 JIONI
11
TABORA NA SINGIDA OFISI YA OCD NZEGA 21-24 /09/2013 08:00 ASUBUHI -16:00 JIONI
12
MOROGORO NA DODOMA OFISI YA RPC DODOMA 26-28 /09/2013 08:00 ASUBUHI -16:00 JIONI
13
DSM NA PWANI DSM  POLICE  ACADEMY 01-03 /10/2013 08:00 ASUBUHI -16:00 JIONI

Muhimu:
  • Mwombaji anaruhusiwa kufanya usaili kwenye kituo chochote cha usaili kilicho karibu naye kulingana na tarehe zinavyoonesha kwenye jedwali hapo  juu ili mradi tu awe amejiridhisha kuwa ni miongoni mwa walioitwa kwenye usaili. Jeshi la Polisi halitahusika na lawama yoyote ile kwa mtu atakayekwenda kwenye kituo cha usaili hali ambapo jina lake si miongoni mwa walioitwa kufanya usaili.
  • Mwombaji aliyeitwa kwenye usaili aje na vyeti vyake vyote vya masomo [(Academic Certificate(s)/Results slip(s) & Leaving certificate(s)], nakala halisi ya cheti cha kuzaliwa (Original Birth certificate). Hati ya kiapo cha kuzaliwa haitakubalika.
  • Mwombaji  awe na namba ya simu itakayotumika kumjulisha endapo atachaguliwa..
  • Kila mwombaji aliyeitwa kwenye usaili atajigharamia usafiri, chakula na malazi kwa muda wote wa zoezi la usaili. Pia waombaji waje na kalamu za wino kwa ajili ya usaili wa kuandika.
Ni muhimu sana kwa kila mwombaji kuzingatia muda wa kuanza usaili.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...