
Leo
Jumatatu tarehe 07/10/2013 Chama cha Mapinduzi kinapokea ugeni mkubwa wa
Makatibu Wakuu wa Vyama vya Ukombozi Kusini mwa Afrika. Makatibu Wakuu
hawa wanakuja kuhudhuria Mkutano wa Sita ambao ni mwendelezo wa mikutano
ya aina hii inayofanyika mara mbili kwa mwaka. (hd)
Vyama
vyote vya Ukombozi vitahudhuria Mkutano huu utakaofanyika jijini Dar es
Salaam tarehe 09 Oktoba. Vyama hivyo ni ANC cha Afrika ya Kusini;
FRELIMO cha Msumbiji, MPLA cha Angola; SWAPO cha Namibia; ZANU-PF cha
Zimbabwe na Chama mwenyeji CCM.
Mkutano
wa Makatibu Wakuu utatanguliwa na mikutano ya Jumuiya za Vijana,
Wanawake na Maveterani itakayofanyika Jumanne Oktoba 8, 2013.
Mkutano
wa Sita wa Makatibu Wakuu utahudhuriwa pia na ujumbe kutoka Chama rafiki
cha Kikomunisti cha China utakaoongozwa na Ndugu Ai Ping, ambaye ni
Naibu Waziri anayeshughulikia Idara ya Kimataifa ya Chama hicho.
Pamoja na
mambo mengine Mkutano huu wa Sita wa Makatibu Wakuu wa vyama vya
Ukombozi kusini mwa Afrika utajadili utekelezaji wa maazimio
yaliyopitishwa katika kikao chao cha tano kilichofanyika huko Tshwane,
Afrika ya Kusini mwezi Machi, 2013.
Mojawapo
ya maazimio hayo ni ujenzi wa Chuo cha Pamoja cha Vyama hivi vya
Ukombozi utakaofanyika Ihemi, katika mkoa wa Iringa. Makatibu Wakuu
wanatarajiwa kuzuru eneo la Ihemi tarehe 08/10/2013 kama sehemu ya
maandalizi ya majadiliano ya Mkutano huo wa Sita.
Mkutano huu utafunguliwa rasmi na Ndugu Abdulrahman Kinana, Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi tarehe 09/10/2013.
Imetolewa na :-
Asha-Rose Migiro
KATIBU WA SIASA NA UHUSIANO WA KIMATAIFA
CHAMA CHA MAPINDUZI
KATIBU WA SIASA NA UHUSIANO WA KIMATAIFA
CHAMA CHA MAPINDUZI
No comments:
Post a Comment