*****
MBUNGE wa Nanyumbu, Dustan Mkapa (CCM), anatuhumiwa kujihusisha na
biashara ya uvunaji haramu wa mbao na magogo katika msitu wa hifadhi ya
Mtambaswala uliopo mkoani Mtwara. Aidha amedaiwa kuorodhesha majina ya
uongo ya watu wanaojihusisha na ujangili, ili kufanikisha nia yake ya
kukwepa operesheni ya safisha ujangili inayoendeshwa na Jeshi la
Wananchi wa Tanzania (JWTZ), kwa kushirikiana na askari wa wanyamapori.
Imedaiwa kuwa hatua ya mbunge huyo imesababisha wananchi wa jimbo lake, kuyakimbia makazi yao kutokana na kuhofia kukamatwa.
Hofu hiyo imekuja kutokana na wanajeshi wanaoshiriki kwenye operesheni hiyo kupiga, kujeruhi na kufikia hatua ya kuua watu wawili.
Wakizungumza na RAI Jumatano kwa nyakati tofauti kwa masharti ya kutotajwa majina kwa kuhofia kipigo kinachoendelea kutolewa jimboni humo, baadhi ya wakazi wanaoishi kwenye jimbo hilo walisema kuwa wamehuzunishwa na kitendo cha mbunge wao kuwahusisha na uharibifu wa misitu ya hifadhi.
Imedaiwa kuwa hatua ya mbunge huyo imesababisha wananchi wa jimbo lake, kuyakimbia makazi yao kutokana na kuhofia kukamatwa.
Hofu hiyo imekuja kutokana na wanajeshi wanaoshiriki kwenye operesheni hiyo kupiga, kujeruhi na kufikia hatua ya kuua watu wawili.
Wakizungumza na RAI Jumatano kwa nyakati tofauti kwa masharti ya kutotajwa majina kwa kuhofia kipigo kinachoendelea kutolewa jimboni humo, baadhi ya wakazi wanaoishi kwenye jimbo hilo walisema kuwa wamehuzunishwa na kitendo cha mbunge wao kuwahusisha na uharibifu wa misitu ya hifadhi.
No comments:
Post a Comment