Si rahisi
kuamini, lakini umeshatutoka,
Sengodo
mwana Mvungi, huzuni kutuachia,
Shambulio
la mapanga, ubongo `kuutawanya’,
Nenda
Baba nenda, taifa lanyong’onyea.
Kwa matendo
ya kihuni, uhuni ukafanyiwa,
Hofu kutanda
nchini, hakuna aliye salama,
Usokuwa na makuu, Mvungi kuhujumiwa,
Acha
machozi yatoke, Mvungi umetutoka!
Sitazami
ya kikale, vina kuvipangilia,
Chochote
chenye huzuni, hapa ninakulilia,
Miongoni
mwa walo bora, Mvungi ulitumika,
Pumzika
kwa amani, Mwenyezi atakujazi.
Hukujawa
na tamaa, za kupora na kuiba,
Mema kuyasimamia,
kasoro kututajia,
Taaluma
kueneza, vijana wakafaulu,
Kwa mapigo
ya mapanga, uhai umekutoka!
Umelala
chini chali, pumzi imekukatika,
Huko sote
tutafika, lakini twahuzunika,
Chanzo
cha kifo hakika, ndicho cha kuhuzunisha,
Wametenda
walotenda, Mwenyezi akiwatazama.
Uchungu
uloupata, dhahiri utawarejea,
Hata
kama sio wao, bali wa kizazi chao,
Watakuswa
kwa mwilini, hadi kwa mioyo yao,
Mwenyezi
atasimama, maombi kuyasikiliza.
Yapo mengi
ya kuyataja, Mvungi ulotutendea,
Kwa taifa
na jamii, ni chanzo kukukumbuka,
Twazililia
na nafsi, walokutesa, kukuua,
Hasira za
Mungu wetu, zijibu maombi yetu.
Sasa tunaomboleza,
hapa nukta niiweke,
Vidoleni
kumetweta, jasho na kutetemeka,
Kuamini umekufa,
Mvungi yataka moyo.
Pumzika
Baba yetu, pumzika kwa amani.
Mashaka Bonifas Mgeta,
Dar es Salaam.
CELL: 0754691540
EMAIL: mgeta2000@yahoo.com
Tanzania.
No comments:
Post a Comment