Katika hali isiyokuwa ya kawaida, shabiki mmoja aliyekuwa
akishuhudia mechi katia ya Yanga na Azam, alifariki dunia jana jioni
katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Shabiki huyo alizimia uwanjani mara baada ya Yanga kupata goli la kwanza na la pekee lililofungwa na Didier Kavumbagu.
Shabiki huyo alizimia uwanjani mara baada ya Yanga kupata goli la kwanza na la pekee lililofungwa na Didier Kavumbagu.
Hata hivyo wasamaria wema walimbeba shabiki huyo na kisha kuwekwa
kwenye machela na kupelekwa katika vyumba vya huduma ya kwanza.
Muda mchache baadae vipaza sauti vya Uwanja waTaifa vilisikika vikitangaza kwamba kuna mtu amezimia na kama kuna ndugu au mtu yoyote wa karibu na mtu huyo ajitokeze.
Muda mchache baadae vipaza sauti vya Uwanja waTaifa vilisikika vikitangaza kwamba kuna mtu amezimia na kama kuna ndugu au mtu yoyote wa karibu na mtu huyo ajitokeze.
Kwa mujibu wa Daktari Nassoro Matuzya shabiki huyo ambaye inasemekana
ni wa timu ya Yanga alianza kuishiwa nguvu mara baada ya Yanga kupata
bao ambako alisimama na kushangilia kwa nguvu.
Shabiki huyo alichukuliwa na watu wa msalaba mwekundu na kwenda
kupewa huduma ya kwanza kwenye vyumba maalum uwanjani hapo na taarifa
zimeeleza kuwa mtu huyo alifariki akiwa katika chumba cha huduma ya
kwanza.
Taarifa za uhakika kutoka TFF kwa mtu ambaye hakutaka kutajwa jina
lake kwa madai kuwa yeye sio msemaji, ameshuhudia mwili wa mtu huyo
ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja, na kwamba ulipelekwa
katika hospitali ya Temeke.
Katika mechi hiyo iliyotoa matokeo ya 1-1, Yanga walianza kupata bao katika kipindi cha kwanza dakika ya 14.
Katika mechi hiyo iliyotoa matokeo ya 1-1, Yanga walianza kupata bao katika kipindi cha kwanza dakika ya 14.
Hata hiyvo Azam ilipambana vikali na kurudisha bao katika kipindi cha
pili ikiwa ni dakika ya 82 wakiwa wachezaji kumi baada ya Erasto Nyoni
kutolewa kwa kadi nyekundu kwa kosa la kumtukana muamuzi.
No comments:
Post a Comment