Waziri wa Nchi Ofsi ya Rais, Mahusiano, Stephen Wasira katika moja ya mikutano ya CCM.
Na Mwandishi wetu
WAZIRI wa× Ofisi
ya Rais, Mahusiano na Uratibu, Stephen Wasira, amesema bado ana nia ya
kuwania urais katika uchaguzi mkuu utakaofanyika mwakani.
Kauli hiyo, aliitoa wakati akifanya mahojiano kwenye kipindi cha× Medani za Siasa na× Uchumi kinachorushwa na Star Tv.
Itakumbukwa
Chama Cha Mapinduzi (CCM), kiliwaadhibu makada wake sita akiwemo
Wassira, mwaka mmoja kutojihusisha na masuala ya kampeni za urais.
Katika kipindi cha jana,× Wasira alisema licha ya kupewa adhabu na chama chake kwa kuanza kampeni mapema, bado hajafuta dhamira ya kuwania nafasi hiyo.
Alisema adhabu hiyo ya chama haimzuii kuwania nafasi hiyo, bali imelenga kuzuia makada wa chama hicho kufanya mambo kinyume na taratibu za chama.
“Nia
ya kuwania urais bado ninayo, nitaendelea nayo kulingana na taratibu za
chama, mimi ni mtu safi na nimeanza siasa tangu nikiwa na umri wa miaka
15,” alisema.
Wasira, aliulizwa swali na mtangazaji wa kipindi hicho atawezaje kugombea urais wakati× Katiba inazuia mtu aliyeshatakiwa kwa jinai na yeye alishawahi kushtakiwa.
Waziri huyo alikiri kushtakiwa na× Warioba katika kesi ya uchaguzi, lakini kesi hiyo ni ya madai na si jinai.
“Kesi
zote uchaguzi ni za madai, mtu aliyeshtakiwa kwa madai hazimkoseshi mtu
kuwania urais, kesi ya jinai ndiyo yenye kutoa zuio hilo…..mimi nipo
‘clean’ kwa kuwa nilishtakiwa kwa madai,” alisema.
Alisema
rushwa katika sekta mbalimbali ni hatari kwa maenedeleo ya taifa na mtu
mmoja mmoja hivyo kila mtu anapaswa akichukie na kuipiga vita.
No comments:
Post a Comment