Na Suzan Mwillo, Mwananchi
Posted Jumatano,Marchi11 2015 saa 9:41 AM
Posted Jumatano,Marchi11 2015 saa 9:41 AM
Kwa ufupi
- Asema pia mwanaye mwingine anataka kuwania nafasi hiyo
Dar es Salaam. Mke wa Baba wa
Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, Mama Maria Nyerere amesema kuwa mtoto
wake, Makongoro Nyerere ana haki ya kugombea nafasi ya urais katika
Uchaguzi Mkuu wa Oktoba.
Ijumaa wiki iliyopita, Makongoro alilieleza gazeti
hili kuwa uamuzi wake kuhusu kuwania kiti hicho utajulikana mara
kipenga kitakapopulizwa na CCM.
Kauli ya Makongoro ilitokana na uvumi uliokuwa
umeenea katika mitandao ya kijamii kuwa mtoto huyo wa tano wa mwalimu
Nyerere alikuwa anaandaliwa na watu waliofanya kazi karibu na mwalimu
awanie nafasi hiyo.
Akizungumza na waandishi ya habari nyumbani kwake Msasani jana, Mama Maria alisema mwanaye ana haki ya kugombea.
Mama Maria aliyekuwa ameawaalika waandishi wa
habari kuzungumzia uvumi uliosambaa kuwa amefariki dunia, alitoa kauli
hilo baada ya kuulizwa kama uvumi huo unahusiana na habari kuwa mwanaye
anataka kugombea urais.
Alisema, “Hapana. Hayo mambo hayahusiani na
mwanangu kutaka kuwania urais… yeye ni raia wa Tanzania na hiyo ni haki
yake ya msingi,”
Pia, alidokeza kuwa wakati akizungumza na mwanaye
mwingine juzi baada ya uvumi wa kifo chake, naye alimwambia kuwa anataka
kuwania nafasi hiyo.
Akitoa ufafanuzi kuhusiana na uvumi huo alisema
kuwa, taarifa za uvumi wa kifo chake zilikuwa za furaha kwake na wala
siyo za huzuni kama watu wengi walivyodhania.
“Tumekuwa tukifanya maombi ya kusali na kufunga
kwa siku 40 kabla ya kipindi hiki cha Kwaresima kwa ajili ya kuliombea
taifa na dunia kwa ujumla. Na sasa tunafunga tena, hivyo kwangu jambo
hilo ni majibu ya maombi tunayofanya. Nimefurahia kwa sababu naona
maombi yanafanya kazi. Haya ni majibu, tunasema tumepita
mashetani,”alisema Mama Maria huku akitania kuwa karne hii ni ya kisasa
kweli, hata marehemu anaongea.
Aliongeza; “Baada ya kupokea taarifa hizo, kwa
kuwa nilikuwa nimelala nilichofanya niliamka nikasali…nadhani Watanzania
wanahitaji sana kusali, sala na kazi. Kama Taifa pia tunahitaji kuwa na
siku moja maalumu ya maombi.”
Licha ya kusema kuwa taarifa hizo zilikuwa za
furaha kwake, Mama Maria alisema taarifa hizo zilizua hofu kubwa kwa
familia yake na Taifa zima kwa ujumla.
Alisema juzi mchana alianza kupokea simu kwa wingi tofauti na ilivyo kwa siku za kawaida.
Source: Mwananchi
Source: Mwananchi
No comments:
Post a Comment