ADV

ADV

ADVERTISEMENT CORNER

HUDUMA YA KUKATA TICKET ZA NDEGE ONLINE


SOMA HABARI

SOMA HABARI
Showing posts with label James Mbatia. Show all posts
Showing posts with label James Mbatia. Show all posts

Thursday, September 26, 2013

VYAMA VYA UPINZANI VYAENDELEA NA MKUTANO WA KATIBA MPYA ZANZIBAR HAPO JANA


Mshikamano: Wenyeviti wa vyamba vya upinzani nchini wakishikana mikono kuonyesha mshikamano kabla ya kuanza mkutano kwenye Uwanja vya Kibandamaiti, Zanzibar jana.
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe (kushoto) akiteta jambo la Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, Joseph Mbatia wakati wa mkutano wa kuungwa mkono na wananchi katika upatikanji wa katiba mpya.
Umati: Wananchi waliohudhuria mkutano huo wa kutafuta katiba mpya.
Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba akihutubia wananchi wakati wa mkutano wa kuungwa mkono na wananchi katika upatikanaji wa katiba mpya.
Lipumba akisalimiana na Mbowe.Kwa hisani ya Global Publishers Blog

Monday, September 16, 2013

Wenyeviti wa vyama vya upinzani wakiwa pamoja, na kwa sauti moja.

 

Wenyeviti wa vyama vya upinzani wamekaa pamoja wakipinga muswada wa katiba usipitishwe. Wakuu hao wa vyama mbalimbali vya siasa na wenye ushawishi mkubwa kwa wamanchi wanakutana pamoja kwa jambo moja tu huku kila mmoja akiwa na tofauti na mwenzake. Watasimama pamoja katika hili la katiba lakini wametofautiana kwa mengi na kila mmoja wao ana nia ya kushika hatamu za uongozi wa nchi hii ya Tanzania. Kama wanavyoungana kwa ajili ya kuupinga mswada wa katiba basi wangewekeza kwenye kuondoa tofauti zao ili waungane kwenye uchaguzi. Wote wasarende uongozi wao na katiba zao wachague uongozi mpya wa muungano waweke mgombea mmoja wa urais. Wakifanya hivi naamini watakuwa wanawatendea haki Watanzania na wapiga kura watakuwa na wakati mzuri wa kuchagua viongozi bora na Wananchi wengi watajitokeza kupiga kura kwa kuwa kutakuwa na ushindani wa ukweli. Tutaingia kwenye kupiga kura bila kuwa na uhakika ni nani ataibuka mshindi, na atakayechaguliwa atakuwa anawakilisha wananchi wote.  Utengano wa wanasiasa ndio unaofanya wapiga kuwa wawe wachache. Pengine kupiga kura inakuwa kama si jambo la kishindani, unajua atakayeshinda anatoka chama fulani, so uchaguzi unakuwa kama ushahidi tu. Hii inasababishwa na ubinafsi wa vyama vya upinzania. Tupeni haki ya Demokrasia na sio kututengatenga kadiri mnavyotaka.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...