ADV

ADV

ADVERTISEMENT CORNER

HUDUMA YA KUKATA TICKET ZA NDEGE ONLINE


SOMA HABARI

SOMA HABARI
Showing posts with label DRC. Show all posts
Showing posts with label DRC. Show all posts

Friday, March 20, 2015

Mvutano kati ya UN na DRC unaendelea

Picha inaonyesha helikopta ya mashambulizi ya MONUSCO, nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya congo.
Picha inaonyesha helikopta ya mashambulizi ya MONUSCO, nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya congo.
Na RFI
Mvutano baina ya Umoja wa Mataifa na serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) umechukuwa sura nyingine hapo jana katika Baraza la Usalama la umoja huo kuhusu kuondoka au la kwa vikosi vya kulinda amani nchini humo MONUSCO.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Congo Raymond Tshibanda amesema kuwa wakati umefika kwa nchi yake kuwajibika kikamilifu kwa ajili ya usalama wa nchi yake akiliomba baraza hilo kuheshimu dhamira ya serikali ya Kinshasa kwa kuamuru MONUSCO waanze kuondoka kwa awamu.
Aidha, waziri huyo amesema kuwa maendeleo ya kisiasa na kiuchumi yaliyoletwa na serikali yake ni mafanikio makubwa, huku akidai kuwa makabiliano ya vikosi vya serikali dhidi ya waasi wa Kihutu wa Rwanda wa FDLR mashariki mwa DRC yanaendelea kushika kasi.(P.T)
Akizungumza kwa niaba ya Umoja wa Mataifa, mwakilishi maalum wa katibu mkuu wa Umoja wa mataifa na mkuu wa vikosi hivyo vya MONUSCO, Martin Kobler, amesisitiza kwamba kwa ujumla hali ya usalama imeimarika na kwamba bado yako maeneo mengi ya kufanyia kazi mashariki mwa nchi hiyo ambako raia wanaishi katika hofu.
Kulingana na vyanzo vya kidiplomasia, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lina mpango wa kupunguza vikosi hivyo kwa kiwango cha askari elfu mbili kati ya elfu ishirini walioko Congo wakati serikali ya Kinshasa ikisema kiwango cha kwanza cha wataokaoondoka kitakua cha askari elfu sita.

Sunday, May 11, 2014

Rais Kikwete awatia moyo Samata na Ulimwengu huko DRC


RAIS wa Jamhuri ya Muungano Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete jana amewatembelea washambuliaji wawili Watanzania wanaocheza TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Mbwana Ally Samatta na Thomas Emannuel Ulimwengu.
Tovuti ya TPM imeandika kwamba Rais Kikwete aliwatembelea wachezaji hao leo mjini Kinshasa ambako wapo na timu yao kwa ajili ya mchezo wa Ligi Kuu ya DRC dhidi ya mahasimu wao katika mbio za ubingwa AS Vita.
Rais Kikwete akiwa na Samatta kulia na Ulimwengu kushoto mjini Kinshasa jana
Rais Kikwete aliye ziarani DRC, alikuwa ameambatana na maofisa wawili wa Ubalozi wa Tanzania majira ya Saa 6:15  mchana alipokutana na wachezaji hao pamoja na Mwenyekiti  wa klabu yao, Moses Katumbi.
Rais Kikwete yupo Kinshasa tangu jana usiku kwa ziara maalum ya Saa 24 juu ya ushirikiano wa DRC na Tanzania, ambako alikutana na rais mwenzake wa huko, Joseph Kabila.
Kikwete alitumia robo saa kuzungumza na akina Samatta katika hoteli ya Congo River, ambako wameweka kambi kwa ajili ya mechi ya kukata na shoka kesho.


Rais Kikwete aliwakumbusha Samatta na Ulimwengu kwamba, Watanzania wanajivunia kuwaona wakiwa na jezi za TPM na kwamba wao ni tegemeo la timu ya taifa, Taifa Stars kwa sasa.

Tuesday, December 3, 2013

UN: Kutumia ndege zisizo na rubani DRC

131123051035_china_stealth_drone_304x171_itcjdbynet_nocredit_9697c.jpg
Majeshi ya Umoja wa Mataifa katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo yameanza kutumia ndege zisizo na rubani kuchunguza harakati za waasi katika mipaka na Rwanda na Uganda.
Hii ni mara ya kwanza kwa majeshi ya Umoja wa Mataifa kutumia ndege za aina hiyo.
Ndege mbili za kwanza zilirushwa kutoka mji wa mashariki wa Goma ambao mwaka jana ulikaliwa kwa muda mfupi na waaasi wa kundi la M23.
Ndege mbili za kwanza zinaundwa na shirika la Italia la Selex ES.
Jeshi la Umoja wa mataifa katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo ndio kubwa kupita yote duniani na lilichangia kwa kiasi kikubwa mwezi uliopita ushindi dhidi ya waasi wa kundi la M23;lakini bado kuna makundi mengine kadhaa ya wanamgambo nchini humo.
Kikosi kipya kilichoimarishwa nguvu cha Umoja wa Mataifa kilitumia ndege za helikopta kulisaidia jeshi la Congo dhidi ya waasi hao wa M23.
Eneo tajiri la madini la mashariki mwa Congo limekumbwa na vita kwa kipindi cha miongo miwili iliyopita lakini kushindwa kwa M23 kumeleta matumaini fulani ya kupatikana utulivu zaidi kwa eneo hilo.(P.T)

Thursday, November 28, 2013

Tanzania, DRC, Burundi zaanzisha ushirikiano

Burundiclip_efd99.jpg
Wakati Kenya, Rwanda na Uganda zimeunda umoja unaoitwa 'Umoja wa Walio Tayari' , Tanzania, Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC) nazo zimeanzisha ushirikiano baina yao.
Katika siku za karibuni kumekuwa na mtikisiko ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) baada ya Tanzania na Burundi kutengwa na wenzao wa Kenya, Rwanda na Uganda katika baadhi ya masuala muhimu ya ushirikiano hasa wa kiuchumi.
Tanzania, Burundi na DRC nazo zimekutana ikiwa ni utekelezaji wa ahadi ya Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta ambaye aliliambia Bunge lililopita kuwa Tanzania inafikiria kushirikiana na nchi hizo.
Mkutano wa ujirani mwema
Akizungumza na waandishi wa habari baada ya mkutano wa Ujirani Mwema uliofanyika mjini Bujumbura, Burundi jana, Sitta alisema Tanzania, Burundi na Kongo zimekubaliana kuendeleza miundombinu ya barabara, reli, anga na usafiri wa maji katika Ziwa Tanganyika.
Alisema mkutano huo ulilenga kuboresha miundombinu ya usafiri katika Ziwa Tanganyika ambalo linaziunganisha Burundi Tanzania, DRC na Zambia.
"Pia tumepanga kuendeleza reli ya kati kutoka eneo la Uvinza, Tanzania hadi Msongati, Burundi na pia kuunganisha Barabara ya Manyoni - Tabora - Kigoma kupitia Bujumbura hadi Kivu ya Kusini, DRC," alisema Sitta.
Mkutano huo ulihudhuriwa na Sitta pamoja na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki wa Burundi, Leontine Nzeyimana na Waziri wa Uchukuzi wa DRC, Jack Lukeba.
"Pia tulitembelea Bandari ya Kalindo iliyoko katika Ziwa Tanganyika upande wa Burundi kwani tunataka kuboresha bandari za ziwa hilo," alisema Sitta.
Waziri huyo alisema Tanzania na Burundi zitaunganishwa na Barabara ya Manyoni – Tabora - Kigoma na Barabara ya Manyovu - Mgina, Mabanda - Bujumbura itakayounganishwa mpaka Kivu ya Kusini, DRC.
Kuhusu usafiri wa anga, Sitta alisema nchi hizo zinaangalia uwezekano wa kuanzisha safari za ndege za Dar es Salaam mpaka Bujumbura.
Muungano wa Walio Tayari
Marais Paul Kagame wa Rwanda, Uhuru Kenyatta wa Kenya na Yoweri Museveni wa Uganda wamefanya vikao vitatu mwaka huu kujadili ushirikiano miongoni mwa nchi zao ambao umepewa jina la Muungano wa Walio Tayari. Kwanza walikutana Juni 24 – 25, mjini Entebbe, Uganda kisha Agosti 28, mjini Mombasa, Kenya na Oktoba 28, mjini Kigali, Rwanda.
Katika vikao vyao iliamuliwa nchi hizo zishirikiane katika kuboresha miundombinu, uanzishwaji wa himaya moja ya ushuru wa forodha, uhamiaji na kuundwa kwa shirikisho kisiasa.
Tanzania yaja juu
Akilihutubia Bunge Novemba 7, mwaka huu mjini Dodoma, Rais Jakaya Kikwete alieleza Tanzania kutofurahishwa na nchi hizo kuanzisha umoja huo na kuitenga bila ya kuwapo kwa sababu za msingi.
Alisema nchi hizo za Kenya, Uganda na Rwanda zimekuwa zikidai kuwa Tanzania haikuwa tayari kutekeleza mambo ya ushirikiano wa EAC ndiyo maana zikaamua kuanzisha ushirikiano baina yao.
Alisema jambo hilo si la kweli huku akidokeza kwamba huenda sababu za nchi hizo kuchukua hatua hiyo ni kutokana na kutofautiana kimsimamo na Tanzania katika masuala ya ardhi, ajira na uhamiaji.
Rais Kikwete alisema nchi hizo zilikuwa zinavunja mkataba wa EAC kwa kukubaliana kushirikiana katika baadhi ya maeneo yaliyokubaliwa na jumuiya.
Aliliambia Bunge kuwa nchi hizo zilikuwa zimekubaliana maeneo manane lakini kati ya hayo, manne yalikuwa yanatakiwa kushughulikiwa ndani ya EAC.
Chanzo:Mwananchi

Sunday, November 3, 2013

ALICHOKIANDIKA KIONGOZI WA KUNDI LA WAASI WA M23 KWENYE UKURASA WAKE WA FACEBOOK MUDA MFUPI ULIOPITA


Kwa muda mufupi sikupatikana kwenye mutandao wa facebook na kwenye simu, sababu nilikuwa mahali hakuna network, kwa sasa nimefika mahali kuna network, Mutaanza pata habari kwa wakati. hatukupigana, tulijitosha katika maeneo zetu bila kupigana, silaha zetu zote tulienda nazo hakuna yenye tuliaca. Ingelukuwa tulikimbiya hatugepata wakati ya kubeba bitu yetu. sasa mutu mwenye anayuwa fanya analyse, aifanye sasa. 1 kwa nini tilijitosha mumaeneo yetu bila kupigana? 2 Tulienda wapi? 3 Tutabakiya kwenye tulienda ama tutarundi, 3 Mbone FARDC haitufwate kwenye tuko? 4 kwa nini Kabila ameitika kuya zungumuza na japo kuwa alisha tushinda? Mwenye kicwa yake haitumike muzuri njo anaeza fanya fete eti M23 imeshindwa. Kwa marafiki, tuko tena tuko. Twasubiri kyenye kitatoka Kampala kwenye mazungumuzo, kama hakuna kizuri kinatoka huko. Na FARDC FDLR, NA MONUSCO inasubutu kuanza Vita tena, PALE MUTAJUWA SISI NI WANANI. — at Bunagana, Democratic Republic of the Congo. 

Friday, September 6, 2013

Taarifa na Taswira Rasmi Kutoka Jeshi la Wananchi wa Tanzania(JWTZ)Kuhusu Ushiriki wa Tanzania Katika Operesheni ya Ulinzi wa Amani nchini DRC,Unatokana na Mgogoro Kati ya Serikali DRC na Waasi hususan Kikundi cha Waasi cha M23.


 Msemaji wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Meja Erick Komba akiongea na waandishi wa habari  leo katika ukumbi wa mikutano uliopo makao makuu ya Jeshi hilo  jijini Dar es Salaam kuhusu ushiriki wa Tanzania katika operesheni ya ulinzi na amani katika nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC). Tanzania ni moja kati ya nchi tatu zilizopeleka kikosi chake nchini DRC ikiwa ni sehemu ya SADC standby brigade inayotoa mchango wake katika Jeshi la Umoja wa Mataifa (MONUSCO) na kinafanya kazi chini ya Force Commander huku majukumu yake yakiwa ni kuzuia waasi kujitanua, kuvunja nguvu ya waasi na kuwapokonya silaha makundi yote ya waasi. Kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Habari (Maelezo) Assah Mwambene.
Mkurugenzi wa Idara ya Habari (Maelezo) Assah Mwambene akiongea na waandishi wa habari jinsi baadhi ya vyombo vya habari vinavyoandika taarifa zisizo  sahihi  kuhusu  ushiriki wa  majeshi ya Tanzania katika operesheni ya ulinzi na amani katika nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) ikiwa ni sehemu ya SADC standby brigade inayotoa mchango wake katika Jeshi la Umoja wa Mataifa (MONUSCO)  . Kushoto ni Msemaji wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Meja Erick Komba.
 Mkurugenzi wa Idara ya Habari (Maelezo) Assah Mwambene (kulia) akimuonyesha kitu Msemaji wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Meja Erick Komba wakati wa mkutano na waandishi wa habari  uliofanyika   leo katika ukumbi wa mikutano uliopo makao makuu ya JWTZ jijini Dar es Salaam.  Mkutano huo uliongelea juu ya ushiriki wa Tanzania katika operesheni ya ulinzi na amani katika nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).  
 Mwandishi wa Habari na Mpiga picha Mwandamizi wa kituo cha Televisheni  cha channel 10 Kibwana Dachi akiuliza maswali  wakati wa mkutano uliofanyika   leo katika ukumbi wa mikutano wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi  wa Tanzania (JWTZ) jijini Dar es Salaam.  Mkutano huo uliongelea juu ya ushiriki wa Tanzania katika operesheni ya ulinzi na amani katika nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).  Wanaomsikiliza kwa makini ni Msemaji wa JWTZ Meja Erick Komba (kushoto) na Mkurugenzi wa Idara ya Habari (Maelezo) Assah Mwambene(kulia).Picha na Lorietha Laurence-Maelezo
--

Simu ya Mdomo  :                                                                      DSM  22150463        
                                                                                             Sanduku la Posta 9203,
Telex                     : 41051                                                                    DAR ES SALAAM, 06 Sep 

Ushiriki wa Tanzania katika Operesheni ya Ulinzi wa Amani nchini DRC, unatokana na mgogoro kati ya Serikali DRC na waasi hususan kikundi cha waasi cha M23. Mgogoro huo ulianza mwezi Aprili 2012 ambapo kikundi cha M23 kilijitoa katika Jeshji la serikali ya DRC na kuanzisha mapigano hali iliyopelekea hali ya usalama nchini DRC kuwa mbaya.

Kufuatia hali hiyo mbaya ya usalama, wakati wa kikao cha International Conference on the Great Lakes Region kilichofanyika tarehe 12 Julai 2012 mjini Addis Ababa, Ethiopia, Mhe. Rais Joseph Kabila aliwasilisha ombi kwa Wakuu wa Nchi za Maziwa Makuu ambazo Rwanda, Uganda, Tanzania,  na DRC akaomba nchi wanachama wa Maziwa Makuu zisaidie kuwapokonya silaha waasi wa M23.

Wakuu wa nchi za Maziwa Makuu walikubaliana na ombi hilo na kutoa maelekezo kwa Mawaziri wa Ulinzi ambao walikutana tarehe 01 hadi 2 Agosti 2012  na kujadili maelekezo ya Wakuu wa nchi za Maziwa Makuu. Mawaziri wa Ulinzi walikubaliana kuwa ni muhimu kwa vikundi vyote vya Waasi (ADF, FDLR na M23) kushughulikiwa na wakawasilisha mapendekezo yao kwa Wakuu wa Nchi za Maziwa Makuu.

Tarehe 7 Agosti 2012, Wakuu wa nchi za Maziwa Makuu walikutana tena mjini Kampala, Uganda na kupanga mkakati wa kuanzishwa kwa ‘Neutral Intervention Force (NIF)’ na nchi wanachama wa Nchi za Maziwa Makuu zikaombwa kuchangia askari watakaounda ‘Neutral Intervention Force (NIF)’ ambapo Tanzania iliombwa na ikahadi kuchangia kikosi kimoja. Kikao hiki kilitoa maelekezo ya hatua inayofuata kwa Mawaziri wa Ulinzi wa Maziwa Makuu.

Tarehe 7 hadi 8 Sep 2012, Mawaziri wa Ulinzi wa maziwa Makuu, walikutana na kujadili utekelezaji wa uanzishwaji wa ‘Neutral Intervention Force (NIF)’. Wakaunda ‘Military Assessment Team (MAT)’ kufanya tathmini ya tishio. Timu hiyo ililifanya tathmini na kuwasilisha taarifa yake kwenye kikao cha Mawaziri wa Ulinzi kilichofanyika tarehe 25 Oktoba 2012 mjini Goma, DRC na baadaye taarifa hiyo iliwasilishwa kwa Wakuu wa Nchi za Maziwa Makuu ambao waliagiza kushirikishwa kwa nchi wanachama wa Jumuiya ya maendeleo kusini mwa Afrika (SADC), Umoja wa Afrika(AU) na Umja wa Mataifa(UN) ili kufanikisha mkakati huo.

Nchi wanachamma wa SADC na Nchi za Maziwa Mkuu kwa pamoja walikubaliana na kupendekeza SADC Standby Brigade ipelekwe DRC kama ‘Neutral Intervention Force (NIF)’. Kufuatia ridhaa hiyo nchi wanachama wa SADC ziliombwa kuchangia ambapo nchi mbalimbali wanachama zilikubali kuchangia, lakini Umoja wa Mataifa(UN) ilizipitisha nchi za Tanzania, Afrika Kusini na Malawi kuchangia askari nguvu ya Brigedi moja kuunda NIF ya MONUSCO.

Aidha, Umoja wa Mataifa mwezi Januari 2013 uliridhia mapendekezo ya Wakuu wa Nchi za Maziwa Makuu na Nchi wanachama wa SADC ya kuundwa ‘Neutral Intervention Force (NIF)’ na kupelekwa DRC. Kufuatia idhini hiyo tarehe 28 Machi 2013, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lilipitisha     Azimio (Resolution) namba 2098 (2013) na kutoa jukumu maalumu la ulinzi wa amani nchini DRC, likijumuisha ushiriki wa Neutral Intervention Force (NIF) kama sehemu ya MONUSCO, na ikaitwa ‘Force Intervention Brigade (FIB)’ ambayo kikosi cha Tanzania ni sehemu ya Brigade hiyo.

Kwa mantiki hiyo ieleweke kwamba, Kikosi cha Tanzania kilichopo DRC ni sehemu ya SADC standby brigade iliyotoa mchango wake katika Jeshi la Umoja wa Mataifa (MONUSCO). Kinafanya kazi chini ya Force Commander, MONUSCO na majukumu yake ni:
    1. Kuzuia waasi kujitanua (Prevention of Expansion)
    2. Kuvunja nguvu za waasi (Neutralization)
    3. Kuwapokonya silaha makundi yote ya waasi.

Kwa kuzingatia kuwa kikosi chetu kiko chini ya majeshi ya Umoja wa Mataifa ya MONUSCO, inamanisha kuwa Operesheni hiyo ni ya Umoja wa Mataifa,  Tanzania haipigani na M-23 na haina tatizo na Rwanda kuhusiana na Operesheni hiyo na ridhaa ya kikosi chetu kwenda DRC ilikubaliwa pia na Rwanda, nchi ambayo ni mwanachama wa nchi za Maziwa Makuu. Aidha, Rwanda imesaidia sana kwa kuruhusu kikosi cha Tanzania kupitisha watu, vifaa na zana katika nchi yake kupeleka DRC.

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Habari na Uhusiano
Makao Makuu ya Jeshi.
Dar es Salaam.

Saturday, July 13, 2013

"TUTAKUCHAKAZA WEWE KAGAME NA RWANDA YOTE KAMA UKITHUBUTU KUTUCHOKOZA".....TANZANIA YAMJIBU RAIS KAGAME


SERIKALI ya Tanzania imeipa onyo kali nchi ya Rwanda ikiitaka isijaribu kuota ndoto za kuishambulia kijeshi, vinginevyo itajibu mapigo kwa nguvu zote na kuhakikisha kuwa imeichakaza.


Kauli hiyo ya kwanza nzito imetolewa jana na Wizara ya Mambo ya Nje ya Ushirikiano wa Kimataifa kufuatia taarifa ya matamshi makali yanayodaiwa kutolewa na Rais Paul Kagame wa Rwanda, dhidi ya Rais Jakaya Kikwete na kutishia kuishambulia Tanzania.


Akizungumza na Tanzania Daima jana jijini Dar es Salaam, Msemaji wa wizara hiyo, Mkumbwa Ally, alisema ingawa Serikali ya Tanzania hadi sasa inajua haina ugomvi wowote na Rwanda, lakini amekiri kuwapo kwa kile alichokiita ‘kupishana lugha’ kwa Rais Jakaya Kikwete na Paul Kagame.


Mkumbwa alikiri Serikali ya Tanzania kunasa matamshi yanayodaiwa kutolewa na Rais Kagame katika moja ya hotuba zake aliyoitoa Juni 30, nchini kwake wakati akihutubia katika hafla moja ya vijana.


Kwa mujibu wa hotuba hiyo, ambayo kwa wiki sasa imesambazwa katika baadhi ya mitandao ya kijamii, Kagame anadaiwa kusikika akitoa matamshi ya vitisho dhidi ya Rais Kikwete, kwamba anamsubiri katika wakati aujuao na kumchapa.


Baadhi ya maneno yanayodaiwa Rais Kagame aliwaambia vijana waliokutana katika mkutano wao uliojulikana kama ‘Youth Konnect’ na kufadhiliwa na mke wake, Janet Kagame, yanasema: “Huyu mtu mliyemsikia akiwa upande wa Interahamwe na FDLR na akashauri majadiliano….majadiliano?”


Aidha, Kagame anadaiwa kusema kuwa hatakuwa tayari kujadili jambo hilo, isipokuwa atamsubiri Rais Kikwete sehemu muafaka na ‘kumtandika’.

“Sitapoteza muda wangu kumjibu Kikwete, inajulikana maana kuna mahali hataweza kuvuka…haiwezekani,” alikaririwa akisema Rais Kagame, akilenga kumtisha Rais Kikwete.


Mbali na Kagame, baadhi ya viongozi kadhaa wa serikali ya Rwanda wamekuwa wakimshambulia Rais Kikwete wakimpachika majina ya kejeli ya; “Rais mhurumia magaidi, wauaji wa kimbari, mkorofi na mwenye dharau.”


Mkumbwa hata hivyo alisema Serikali ya Tanzania haina sababu ya kuingia katika vita na Rwanda, kwa sababu tu ya ushauri alioutoa Rais Kikwete wa kuitaka ikutane na wapinzani wake wanaoishi ndani ya nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), kujadiliana kuhusu amani ya nchi za Maziwa Makuu.


Alisema msimamo wa Tanzania utabaki kuwa uleule wa kuitaka nchi hiyo ikubali kukaa meza moja na wapinzani wake, ili kumaliza migogoro inayoendelea katika nchi hizo za maziwa makuu, ambao unaungwa mkono na jumuiya ya kimataifa na SADC.

“Unajua mgogoro wa DRC na Rwanda hauwezi kumalizika bila ya nchi hizo kukaa meza moja na wapinzani wao ili kupata suluhu ya kudumu,” alisema Mkumbwa.


Aliwataka Watanzania kuwa watulivu na kuendelea na kazi zao kama kawaida, kwani serikali yao iko makini katika kulinda mipaka yake.

Chanzo cha mzozo
Msuguano baina ya nchi hizi mbili ulianza siku chache tu baada ya kumalizika kwa kikao cha viongozi wa nchi za Maziwa Makuu na ambacho kilihudhuriwa pia na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon, chini ya uenyekiti wa Rais wa Uganda, Yoweri Museveni.

Rais Kikwete wakati akimtaarifu Rais Museveni kile walichokuwa wamekijadili katika kikao hicho kwa vile aliketi kwa muda kwa kuwa alichelewa kuwasili, alisema ni vema serikali za Rwanda na Uganda zifungue mlango wa mazungumzo na waasi wao na akaanza kutaja majina ya vikundi vya uasi vya nchi hiyo vilivyopo nchini DRC.

Habari zinasema kauli ya Rais Kikwete iliungwa mkono na Rais Museveni akisema: “Bila mazungumzo hatutafika popote pale”.  


Hata hivyo, matamshi hayo yalijibiwa kwa ukali na serikali ya Rwanda, kiasi cha kumlazimu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, kutoa tamko bungeni.


Kwa kauli yake, Membe alisema serikali ilikuwa imeshangazwa na shutuma hizo za Rwanda kwani halikuwa jambo baya kutoa ushauri uliolenga kuleta mapatano na kuepusha umwagaji zaidi wa damu wa wananchi. 

Akaongeza kuwa, ilikuwa ni wajibu wa Serikali ya Rwanda kuupokea ama kuukataa, na wala si kutoa maneno ya kejeli na vitisho.

Kauli ya Zitto
Akizungumzia kauli hiyo ya vitisho, mwanasiasa machachari hapa nchini na Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Zitto Kabwe, alisema ushauri wa Rais Kikwete kwa Rwanda ulikuwa wa busara mno na akashangaa kuona nchi hiyo jirani ikitoa vitisho, kejeli, dharau na ukosefu wa adabu kwa Kikwete.
 
Katika moja ya tamshi lake alilolitoa jana katika mitandano ya kijamii, Zitto ambaye ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini (CHADEMA) alisema Marekani wanaongea na waasi wa kundi la Taliban, hivyo hakuna dhambi kwa Rwanda pia kufanya hivyo.

“Pia kama hutaki ushauri si unakataa tu, sasa kuanza kurushiana maneno ya nini tena? Hutaki ushauri basi. 

Maneno ya kila siku ya nini? Tangu Kikwete amesema kule Addis, hajasema tena. Membe (waziri) akajibu Dodoma Tanzania haijasema tena. Kigali inasema mambo haya kila siku kwa ajili ya nini?


Taliban na Al Qaeda si wale wale? Wale watoto waliozaliwa mwaka 1994 na wakimbizi wa Kihutu waliopo Kongo nao ni wauaji? Tufikiri vizuri mambo haya. Kuna ‘genociders’ wasakwe, wakamatwe wahukumiwe. Kuna watu wana haki kabisa ya kutaka kushiriki kwenye siasa za Rwanda na wanazuiwa, wameshika silaha. Hawa lazima wakae meza moja wakubaliane,” alisema Zitto.

Mwanasiasa huyu alisema kwa sasa serikali za nchi hizo mbili zinatakiwa kuingia katika vita ya kupambana na kuondoa umasikini wa watu wake na si vita ya mtutu wa bunduki.

Busara itumike kwa viongozi ‘neutral’ kama Uhuru Kenyatta kuwaweka pamoja Kagame na Kikwete wamalize tofauti zao. Haya maneno hayana maana yoyote,” alisema.

Alisema vita haitamuumiza Rais Kagame wala Rais Kikwete na familia zao, bali itaumiza wananchi wa kawaida wa mikoa ya Kagera na Kigoma na mikoa ya mpakani ya Rwanda.


Vita itaturudisha nyuma sana kwenye juhudi za maendeleo. Vita itazima harakati za kujenga demokrasia nchini.  Busara itumike tu,” alisema Zitto.

Tanzania Daima

Read more: http://talkbongo.blogspot.com/2013/07/tutakuchakaza-wewe-kagame-na-rwanda.html#ixzz2Yt6pToyQ
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...