ADV

ADV

ADVERTISEMENT CORNER

HUDUMA YA KUKATA TICKET ZA NDEGE ONLINE


SOMA HABARI

SOMA HABARI

Sunday, December 2, 2012

Afunga ndoa na kuishi na mwanaume kwa miaka 19 akijua kuwa ni mwanamke




 
Raia mmoja wa Ubelgiji aliyetambulika kwa jina moja tu Jan, amekuwa akifanyiwa matibabu ya akili  baada ya kuathirika kisaikolojia baada ya kugundua kuwa mwanamke aliyefunga naye ndoa miaka 19 iliyopita alikuwa ni mwanaume aliyejibadilisha jinsia. Jan mwenye umri wa miaka 64 kwa sasa amekuwa akilalamika kutaka kuachana na mwanamama hiyo. Hata hivyo jaribio la kisheria la kutaka kuachana na janajike hiyo lakini amegonga mwamba kwa kuwa mahakama moja ya Ubelgiji imekataa hadi sasa kutengua ndoa hiyo kwa kuwa mama huyo (Monica) anatambulika kisheria kama mke wa ndoa. Bwana Jan amejitetea kwamba Monica raia wa Indonesia walikutana mwaka 1993 na kujiridhisha kuwa ni mwanamke mrembo na bora wa kuwatunza watoto wake na hata kuzaa naye watoto. Jana anadai kuwa Monica alitumia nyaraka za uongo na majina feki ili kukamilisha azma yake ya kuolewa na aweze kuishi kama mwanamke. Jan alimuoa Mocica baada ya mkewe wa awali kufariki na kumwachia watoto wawili ambao walikuwa wakiishi naye kwa ukiwa na ndipo alipoamua kumwoa Monica, alisema mwanasheria wa Jan Verjau Liliane.


Jan, alisema kuwa yeye na mke wake  Monica walliamua kuoana na wakakubaliana kutokuwa na watoto kwani yeye tayari alikuwa na watoto wawili na mke wake ambaye alishafariki. Jan aliendelea kusema kwamba Monica alikuwa akimdanganya na wakati mwingine alikuwa akitumia pedi kujikinga na damu ya hedhi ili kuficha ukweli. "Hata wakati wa ngono, mimi kamwe sikuona kitu chochote tofauti na mwanamke" alisema.

Kwa miaka yote hiyo 19 wanandoa hao walikuwa wakiishi kwa maisha ya kawaida ya furaha, na Monica alikuwa kama dada mkubwa wa watoto wake hadi ndoa yao ilipoanza kuingia katika mkwaruzo hasa pale Monica alipopata ajira.
“Monica alianza kubadilika sana” alisema Jan
Wakati mwingine mwanangu mkubwa alikutana na Monica (mama yake wa kambo) kwenye clab za muziki za usiku akiwa amevalia nguo fupi sana na t-shirt iliyoacha tumbo wazi hadi kwenye kitovu.

Hata hivyo fununu zilianza kuzagaa kuwa Monica alikuwa ni mwanume aliyejibadilisha jinsia. Mwanangu aliweza kunasa mawasiliano yake na wanaume wenzake kwenye komputa yake na ndipo tulipopata uhakika kwamba Monica niloiyeishi naye kwa miaka 19 hakuwa mwanamke bali mwanaume aliyefanyiwa opereshini na kuwekewa maumbile ya kike.

Nilipopata uhakika huu nilikasirika sana. “Nilimsukuma kwenye ukuta wa nyumba yetu kwa hasira sana” Sasa nimegundua kuwa Hon ambalo ndo jina lake halisi alikuwa sio mwanamke halisi. Baada ya mzozano mkali Hon alikiri kwamba kweli yeye hakuwa mwanamke kwani alizaliwa kama mvulana na kwamba ailifanyiwa upasuaji na kubadilishwa kuwa mwanamke.
Hata hivyo mzozo ule ulipelekewa kupigwa simu polisi na ndipo kesi ya kutengana naye ikaanza.


 
 
Siku yao ya ndoa
 

Habari hii imetafsiriwa na mdau wa golden blogspot kutoka mtandao wa telegraph
Ukitaka kuisoma kwa Kiingereza bofya hapa:
 http://www.telegraph.co.uk/news/worldnews/europe/belgium/9703166/Belgian-discovers-his-wife-used-to-be-a-man-after-19-years.html

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...