Kanye Omari West akiwa na mkewe
Wanamziki Kim na Kanye wesr wamekataa offa ya dola milioni 3 kwa magazeti ya habari has yale ya udaku wa kimataifa kuwa wa kwanza kupiga picha ya mtoto wao atakayezaliwa hivi karibuni. Inaonekana Kim Kardashian hapendi kufuata nyayo za mastaa wenzake kama Aina Jolie na Jessica Alba na Christina Aguilera ambao walilipwa mahela kibao kwa watoto wao kupigwa picha. Kulingana na chanzo cha habari cha TMZ cha huko Marekani wapenzi hao wameamua kutokuiuza picha ya mtoto wao walao kwa sasa. Sijui kama watakuja kukubali baadaye au wanajifanya kukataa ili dau lipande zaidi.
Kim Kardashien ambaye ni mjasiriamali, mwanamitindo na mtayarishaji wa kipindi cha Kardeshien reality show alikuwa akilipwa dola 5,000 kwa kipindi lakini baada ya kipindi chake kuwa cha mafanikio makubwa sasa analipwa dola 80,000 kwa siku. Hivyo utajiri wake kwa sasa unakadiriwa kufikia $ milioni 40
JUMBA LA KIM
Mwaka 2010 Kim alinunua jumba la dola milioni 4.8 Beverly Hills. Jumba hilo lina vyumba vya kulala 5 na ukubwa wa eka nne. Ni eneo wanaloishi matajiri wakubwa sana.
FERRARI YA KIM
FERRRI YAKE YA ZAMANI
Kwa upande wake Kanye Omari West mwenye umri wa miaka 35, ana utajiri wa dola milioni 90 na majumba na magari yasiosemekana
Jumba la Kanye Omari West
Gari la Kanye West likiendeshwa na mkewe
No comments:
Post a Comment