ADV

ADV

ADVERTISEMENT CORNER

HUDUMA YA KUKATA TICKET ZA NDEGE ONLINE


SOMA HABARI

SOMA HABARI

Thursday, June 6, 2013

Uongozi wa CCM Wakutana Kwa Mazungumzo na Ujumbe wa Chama Cha Kikomunisti cha Vietnam (CVP)


 .Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akimkaribisha katika hoteli ya Protea Cortyard jijini Dar es Salaam, Mjumbe wa Kamati Kuu na Mwenyekiti wa Mambo ya Nje wa Chama Cha Kikomunisti cha Vietnam Hoang Quan, baada ya mgeni huyo na ujumbe wake kuwasili kwa ajili ya mazungumzo na Kinana, jana, Juni 6, 2013.
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akimkaribisha katika hoteli ya Protea Cortyard jijini Dar es Salaam, Mjumbe wa Kamati Kuu na Mwenyekiti wa Mambo ya Nje wa Chama Cha Kikomunisti cha Vietnam Hoang Quan, baada ya mgeni huyo na ujumbe wake kuwasili kwa ajili ya mazungumzo na Kinana, jana, Juni 6, 2013.
Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Philip Mangula akimpa zawadi ya sanamu ya twiga iliyotengenezwa  kwa vyuma chalavu, Mjumbe wa Kamati Kuu na Mwenyekiti wa Mambo ya Nje wa Chama Cha Kikomunisti cha Vietnam Hoang Quan, wakati wa chakula cha mchana kwenye mgahawa wa Akemi, jijini Dar es salaam. Sanamu hiyo ni ubunifu unaofanywa na kikundi cha walemavu jijini Dar es salaam
 Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akimshukuru Mjumbe wa Kamati Kuu na Mwenyekiti wa Mambo ya Nje wa Chama Cha Kikomunisti cha Vietnam Hoang Quan, baada ya mazungumzo yao katika hoteli ya Protea Courtyard, Dar es salaam, leo. Kushoto ni Dk. Asha Rose Migiro na watatu kushoto ni Nape Nnauye.
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana  (wapili kulia) akizungumza na Mjumbe wa Kamati Kuu na Mwenyekiti wa Mambo ya Nje wa Chama Cha Kikomunisti cha Vietnam (CVP), Hoang Quan (wapili kulia), katika hoteli ya Protea Cortyard jijini Dar es Salaam. Jana Juni 6, 2013. Kushoto ni Katibu wa NEC ya CCM, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Dk. Asha-Rose Migiro na Watatu kushoto ni Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye.
Mjumbe wa Kamati Kuu na Mwenyekiti wa Mambo ya Nje wa Chama Cha Kikomunisti cha Vietnam Hoang Quan, akizungumza katika hoteli ya Protea Courtyard, Dar es salaam, jana.
Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Phili Mangula akizungumza wakati wa chakula cha mchana kilichoandaliwa kwa ajili ya ujumbe wa Mjumbe wa Kamati Kuu na Mwenyekiti wa Mambo ya Nje wa Chama Cha Kikomunisti cha Vietnam Hoang Quan (wapili kushoto) katika Mgahawa wa Akemi jijini Dar es Salaam.jana. Picha zote na Bashir Nkoromo

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...