Watu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi, wamewavamia na kuwajeruhi askari
mwenye no G369 PC Mansour na Hv507 PC Mwalimu, wakiwa doria ya pikipiki
ambao walinyang'anywa silaha mbili aina ya SMG no 14301230 na 14303545
na watu wasio julikana mkoani Tanga.
Taarifa ya Jeshi hilo kwa vyombo vya habari imesema tukio hilo limetokea
Januari 26, 2015 majira ya saa 23:30hrs eneo la barabara 04 jijini
humo.
Aidha, imesema mmoja wa majeuhi askari mmoja no H 507 PC Mansour
amejeruhiwa vibaya maeneo mbalimbali ya mwili na amelazwa katika
Hospitali ya Mkoa Bombo.
Katika uchunguzi wa awali Polisi wamefanikiwa kumtia hatia hatiani
mtuhumiwa mmoja, Ayubu Haule, (27), fundi Radio Mkazi waCorner Z Amboni
Kiomoni ambaye alikamatwa eneo la tukio akijaribu kutoroka na pikipiki
na mara baada ya kupekuliwa ndipo alipokutwa na mchoro wa ramani
unaoonyesha matokeo ya Barabara na kufunguliwa kesi yenye no
TAN/IR/322/2015.
Mtuhumiwa anaendelea kuhojiwa na Jeshi hilo huku timu ya Intel na
makachero wa Polisi ikiendelea kufanya doria pamoja na Section 2 za FFU.
No comments:
Post a Comment