Shabiki
mwananke wa Yanga akitolewa kwenda kupata huduma ya kwanza baada ya
kuzimia alipokuwa akishagilia bao la pili dhidi ya watani wao wa jadi
Simba katika mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kwenye Uwanja
wa Taifa, Dar es Salaam leo. Timu hizo zimetoka sare ya mabao 3-3.
Shabiki mwingine wa Yanga akiwa amezimia
Wapenzi wa Yanga wakishangilioa
Kikosi cha Yanga kilichopepetana na Simba
Kikosi cha Simba kilichocheza na Yanga
Shabiki wa Simba akiwa amezimia
SIMBA
SC jana ilitoka nyuma kwa mabao 3-0 na kupata sare ya 3-3 na wapinzani
wao wa jadi, Yanga SC katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara
uliofanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Katika mchezo huo uliochezeshwa na refa Isarel Mujuni Nkongo, hadi mapumziko tayari Yanga SC walikuwa mbele kwa mabao 3-0.
Mrisho Khalfan Ngassa alifunga bao la kwanza dakika ya 15 akimalizia kazi nzuri ya Didier Kavumbangu aliyepiga mpira wa juu uliomchanganya kipa Abbel Dhaira na kudondokea chini kabla ya mfungaji kuusukumia nyavuni.
Katika mchezo huo uliochezeshwa na refa Isarel Mujuni Nkongo, hadi mapumziko tayari Yanga SC walikuwa mbele kwa mabao 3-0.
Mrisho Khalfan Ngassa alifunga bao la kwanza dakika ya 15 akimalizia kazi nzuri ya Didier Kavumbangu aliyepiga mpira wa juu uliomchanganya kipa Abbel Dhaira na kudondokea chini kabla ya mfungaji kuusukumia nyavuni.
![]() |
Betram Mombeki alifunga la kwanza, SImba SC ikapata uhai na kurudisha yote |
Simba
SC ilikuja juu baada ya bao hilo na kujaribu kusaka bao la kusawazisha,
lakini walikuwa ni Yanga tena waliofanikiwa kupata bao la pili dakika
ya 36, mfungaji Hamisi Kiiza aliyeunganisha mpira wa kurushwa na Mbuyu
Twite.
Bao la pili lilionekana kuwachanganya Simba na kuwaacha Yanga wacheze kwa madaha zaidi, pasi nyingi za aina zote na mbwembwe za kila aina.
‘Diego wa Kampala’, Hamisi Kiiza aliifungia Yanga SC bao la tatu dakika ya 45 akimalizia pasi nzuri ya Kavumbangu, ambaye aliipasua ngome ya Simba SC na kubaki na kipa Abbel Dhaira, lakini akaamua kumpa mwenzake amfunge Mganda mwenzake.
Kipindi cha pili, mambo yalibadilika na Simba SC wakaanza kurudisha bao moja baada ya lingine hadi kupata sare ya 3-3.
Bao la pili lilionekana kuwachanganya Simba na kuwaacha Yanga wacheze kwa madaha zaidi, pasi nyingi za aina zote na mbwembwe za kila aina.
‘Diego wa Kampala’, Hamisi Kiiza aliifungia Yanga SC bao la tatu dakika ya 45 akimalizia pasi nzuri ya Kavumbangu, ambaye aliipasua ngome ya Simba SC na kubaki na kipa Abbel Dhaira, lakini akaamua kumpa mwenzake amfunge Mganda mwenzake.
Kipindi cha pili, mambo yalibadilika na Simba SC wakaanza kurudisha bao moja baada ya lingine hadi kupata sare ya 3-3.
![]() |
Hamisi Kiiza alifunga mabao mawili kipindi cha kwanza |
Kipa wa Simba akishukuru mungu baada ya kusawazisha mabao matatu.PICHA ZOTE NA KAMANDA RICHARD MWAIKENDA
No comments:
Post a Comment