ADV

ADV

ADVERTISEMENT CORNER

HUDUMA YA KUKATA TICKET ZA NDEGE ONLINE


SOMA HABARI

SOMA HABARI
Showing posts with label Biashara. Show all posts
Showing posts with label Biashara. Show all posts

Thursday, January 29, 2015

BENKI YA CRDB YAZINDUA KAMPENI YA UTUMIAJI WA SIMBANKING NA FAHARI HUDUMA WAKALA


Mkurugenzi mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei akitoa hotuba yake wakati wa uzinduzi huo.
BENKI ya CRDB imezindua kampeni maalum ya utumiaji wa huduma zake kupitia simu za mkononi 'SimBanking' kupitia kwa mawakala wa 'FahariHuduma'.
Akizungumza jijini Dar es Salaam katika uzinduzi wa kampeni hiyo ijulikanayo kama 'Tuma Pesa na SimBanking Shinda Passo', Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo, Dk. Charles Kimei alisema lengo la kuanzisha kampeni hiyo ni kuwakumbusha wateja wake na watanzania wote kwa ujumla umuhimu wa kutumia njia hizo mbadala ili kupata huduma kwa urahisi na uharaka.
Alisema kampeni hiyo inatarajiwa kutoa magari kumi na mbili ambapo kila mwezi mshindi mmoja atazawadiwa gari hilo, pamoja na zawadi ya gari la wateja watakaotumia huduma hizo pia wataweza kujishindia zawadi nyingine mbalimbali zikiwemo solar power, tables na simu za kisasa za mkononi.
"Tunataka kuwavutia wateja wetu kuziamini na kuzitumia zaidi huduma hizi kwani ni sawa kabisa na kupata huduma kupitia matawi yetu,".
 
 

Wednesday, January 28, 2015

Maneno ya Said Fela kuhusiana kufungwa kwa maduka ya Kariakoo

.
.
 Kufuatia kwa wafanyabiashara wa Kariakoo kufunga maduka yao Jan 27, meneja wa taasisi ya Mkubwa na Wanae, Yamoto Band na Wanaume Family Said Fella ameyatoa ya moyoni kuhusiana na tukio hilo.
Kikubwa ni kuangalia nini tatizo maana wananchi wanasema kwamba wanaonewa kwa hiyo Serikali ifike wakati waangalia wananchi wanaonewa kitu gani, maanake wanasema kule wanapolipa tozo TRA kuna utaratibu wa kulipa  fati yako, la msingi wao wanachogombania kule ni kwamba biashara zote zitumike kwa machine unakuta mtu mwingine mtaji wake mdogo anauza jeans zake saba na shati zake kadhaa ukimwambia anunue machine laki tano au laki tatu huo msingi wake haufanani na hizo hela za kwenda kununua hiyo machine, kwa hiyo naomba Serikali ikae na wananchi wazungumze suala hilo, nchi yetu ya Amani na bado tunaendelea kupenda iwe na Amani“—- Alisema Said Fela akizungumza na millardayo.com.
Hapa kuna sauti ya Said Fela akiongea na millardayo.com, isikilize kwa kubonyeza play hapa.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...